ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, August 11, 2011

AIRTEL YAENDELEA KUPANUA MAWASILIANO NA HUDUMA MPYA MSIMU WA RAMADHANI

•YAFUNGUA HUDUMA ZA MAWASILIANO KANYEZI RUKWA
•OFA YA RAMADHANI BADO INAENDELEA TUMA NENO RAMADHANI KWENDA 15322 SASA...

AGOSTI 11, 2011 Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel imeendelea kukekeleza azimio lake la kutoa huduma bora na bei nafuu nchini kwa kuzindua huduma ya mwasilaino kanyezi mkonia Rukwa wiki hii.

Katika kauli iliyotolewa na Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania Jackson Mmbando alisema, “Airtel imedhamiria kutoa huduma bora na nafuu na kuongeza mtandao wake kwenye maeneo mengi ya mikoani ili kuwapati wateja wake huduma bora za mawasiliano vijijini na maeneo ya miji nchiniTanzania .

“Tunaamini huu ndio wakati muwafaka kuendelea kupanua huduma za mawasiliano mkoani Rukwa pamoja na vjiji vingine, Kuwepo kwa mtando wa mawasiliano Rukwa kutainua shughuli za uchumi na kusaidia wakazi wa Kanyezi na jamii ya Tanzania kwa ujumla” Aliongeza kusema Mmbando

Mmbando alisema Airtel itaendelea kupanua mtandao wake nchini mwaka huu na mkazo utawekwa kwa maeneo ya Vijijini na hasa maeneo ya mikoa ya Pwani, kusini na Mashariki ya Kati.

“Kadri tunavyopanua mtandao wetu ndivyo tunavyo guza jamii na watu tunaowaunganisha kwa kuongeza na kuboresha hali ya maisha kwa kuwezesha na kufanikisha mawasiliano,” alisema Mmbando

“Tunazo timu za wataalum mikoani ambazo zinafanya thathimini ya mara kwa mara, na kila kunapokuwa na mahitaji ya mtandao, itatekeleza inavyotakiwa,” alimalizia kusema Mmbando

Zaidi ya kupanua huduma za mawasiliano Airtel inawakumbusha wateja kuna ofa ya Msimu wa Ramadhani. Wateja wa Airtel wanaweza kujiunga katika huduma hii kwa kutuma neno RAMADHAN kwenda 15322 nakupata ,Mistari ya Kuran, Saa za Ibada ,mida ya kufunga na kufungua, kila siku. Utatozwa sh 500 tu kwa wiki.

Sambamba na hili pia wateja wanazawadiwa muda wa maongezi,sms pamoja na internet Bure kwa kuongeza salio tu kuanzia shilingi 1000 na kuendelea kila siku kuanzia kuanzia saa 5 usiku hadi saa 12 asubuhi. ONGEA USIKU KUCHA

Wateja wetu wa Rukwa sasa nanyi mnaweza kujiunga na huduma hii na kufurahia ofa ya Ramadhani pamoja na wateja wetu wote nchi nzima.




Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.