ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, May 6, 2011

TBL YAKABIDHI VIFAA VYA MICHEZO KITUO CHA MWANZA KWA MAANDALIZI YA KILI TAIFA CUP 2011.

Picha ya pamoja katika makabidhiano ya vifaa vya michezo kwa ligi ya Kili Taifa Cup 2011 ambapo Muhib Kanu meneja timu ya Shinyanga IGEMBESABO (shoto), akipokea vifaa hivyo toka kwa Mwenyekiti wa chama cha soka mkoani Mwanza Jackson Songora (kati) na Ofisa Msimamizi wa mashindano hayo George Wakuganda toka TBL.

Meneja wa timu ya mkoa wa Mara, Chiganga Pascal (shoto) akipokea vifaa toka kwa Mwenyekiti wa chama cha soka mkoani Mwanza Jackson Songora, tayari kwa kuianza ligi ya Kili Taifa Cup 2011, makabidhiano yaliyofanyika leo katika ofisi za uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

Jackson Songora akizungumza wakati wa sherehe za kukabidhi vifaa mbalimbali vya michezo kwa ajili ya Mashindano ya Kili Taifa Cup yanayoanza kesho katika uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza.

Jumla ya timu nne za kituo hiki chenye timu toka mkoa wa Kagera, Mara, Shinyanga na Mwanza zimekabidhiwa vifaa hivyo tayari kushiriki michuano hiyo inayotaraji kuanza kutimua vumbi kuanzia kesho katika vituo vyote nchini.


(Picha na Mohamed Mambo)

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.