Katika ujenzi wa barabara aina hii hutumii simenti labda katika kingo na mifereji yake pembezoni kwaajili ya kupitisha maji, ila barabara yenyewe pale kati ni kuyapanga tu mawe kisha ukajaza udongo kidogo kuyafanya yakae sawia.
Kwa upande wa wananchi wao wanasema kuwa wanaishukuru serikali ya mkoa kwa ubunifu huo, kuwanusuru na makorongo na madimbwi ya maji yaliyokuwa yakisababishwa na maji kutuama yakizua urahisi wa usafiri, usafirishaji na usambazaji huduma hivyo watumie changamoto hiyo kuboresha maisha ya wananchi wake sambamba na maadhari ya jiji.
Barabara ambazo zimetengenezwa kwa kutumia teknolojia hii rahisi inayotumia nguvu shirikishi ya wananchi jijini Mwanza ni pamoja na Kitangiri makaburi, Butimba na Igogo.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.