Wasaidizi wa maafa nchini Hispania wakiwa mtaani katika kijiji cha Cordoba kusini mwa nchi hiyo mbele ya magari yaliyopandiana mara kupitia mvua kubwa zinazoendelea kunyesha nchini humo.
Nako nchini marekani hali ni tete mvua kubwa kama za enzi za Nuhu zanyesha kiasi cha kusababisha watu kuhaha huku na kule kutafuta makazi, miji imejaa maji barabara hazipitiki kama hali inavyoonekana pichani jimboni Mississippi.
Wakati mvua kubwa zikiripotiwa kunyesha sehemu kadhaa hapa duniani hata kusababisha maafa huko nchini India kuna hali ya joto kali kinomanoma linalofikia nyuzi joto degree 49. Pichani kijana mmoja wa nchi hiyo akijipoza majini ndani ya ziwa Srinagar mara baada ya kutokota na joto hilo.
Radi mbaya kuliko inaripotiwa kutokea na kusambaratisha mnara mkuu wa mawasiliano ulioko katika vilima vya Petrin vilivyoko katika jiji la Prague, katika Jamhuri ya Czech.
Jijini Mwanza mvua isiyo na madhara imenyesha majira ya saa saba na nusu, na kudumu kwa muda wa nusu saa. Hali ya hewa kwa sasa imetulia yaani ni safiiiiii.
Kina nani wanaomchagua Papa ajaye na wanatoka wapi?
-
Kufuatia kifo cha Papa Francis mwenye umri wa miaka 88 na mazishi yake
Jumamosi, makadinali kutoka kote ulimwenguni hivi karibuni watakusanyika
Vatican kum...
”Rasmi Soko Kuu la Manispaa ya Bukoba lavunjwa”
-
Soko Kuu la Manispaa Bukoba limevunjwa ili kupisha ujenzi wa soko jipya la
kimataifa unaotarajiwa kuanza muda wowote.
Kwa Wakati tofauti wameonekana Wafa...
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.