Nako nchini marekani hali ni tete mvua kubwa kama za enzi za Nuhu zanyesha kiasi cha kusababisha watu kuhaha huku na kule kutafuta makazi, miji imejaa maji barabara hazipitiki kama hali inavyoonekana pichani jimboni Mississippi.
Wakati mvua kubwa zikiripotiwa kunyesha sehemu kadhaa hapa duniani hata kusababisha maafa huko nchini India kuna hali ya joto kali kinomanoma linalofikia nyuzi joto degree 49. Pichani kijana mmoja wa nchi hiyo akijipoza majini ndani ya ziwa Srinagar mara baada ya kutokota na joto hilo.
Radi mbaya kuliko inaripotiwa kutokea na kusambaratisha mnara mkuu wa mawasiliano ulioko katika vilima vya Petrin vilivyoko katika jiji la Prague, katika Jamhuri ya Czech.
Jijini Mwanza mvua isiyo na madhara imenyesha majira ya saa saba na nusu, na kudumu kwa muda wa nusu saa. Hali ya hewa kwa sasa imetulia yaani ni safiiiiii.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.