Wasaidizi wa maafa nchini Hispania wakiwa mtaani katika kijiji cha Cordoba kusini mwa nchi hiyo mbele ya magari yaliyopandiana mara kupitia mvua kubwa zinazoendelea kunyesha nchini humo.
Nako nchini marekani hali ni tete mvua kubwa kama za enzi za Nuhu zanyesha kiasi cha kusababisha watu kuhaha huku na kule kutafuta makazi, miji imejaa maji barabara hazipitiki kama hali inavyoonekana pichani jimboni Mississippi.
Wakati mvua kubwa zikiripotiwa kunyesha sehemu kadhaa hapa duniani hata kusababisha maafa huko nchini India kuna hali ya joto kali kinomanoma linalofikia nyuzi joto degree 49. Pichani kijana mmoja wa nchi hiyo akijipoza majini ndani ya ziwa Srinagar mara baada ya kutokota na joto hilo.
Radi mbaya kuliko inaripotiwa kutokea na kusambaratisha mnara mkuu wa mawasiliano ulioko katika vilima vya Petrin vilivyoko katika jiji la Prague, katika Jamhuri ya Czech.
Jijini Mwanza mvua isiyo na madhara imenyesha majira ya saa saba na nusu, na kudumu kwa muda wa nusu saa. Hali ya hewa kwa sasa imetulia yaani ni safiiiiii.
Mambo sita kuuelewa msimamo wa Papa mpya
-
Papa Leo alichaguliwa kuwa kiongozi mpya wa Kanisa Katoliki Alhamisi
kufuatia kifo cha mtangulizi wake, Papa Francis, katika kongamano la siku
mbili katika...
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.