ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, May 12, 2011

HAFLA YA KUWAPONGEZA WAANDISHI WA MKOA WA MWANZA WALIOPATA TUZO 2010 MAY 11/2011 ILIVYOFANA.

Emmanuel Chacha wa ITV - Aliyeshinda Tuzo ya Habari Bora ya Biashara kupitia gazeti la Raia Mwema.

Sheilla Sezzy wa Mwananchi - Tuzo ya Habari Bora ya Afya 2010.

Cosmas Makongo wa ITV - Tuzo ya Habari bora ya Biashara 2010-2011 Tuzo anayoishikilia mwaka wa pili mfululizo.

Shughuli ya kuwapongeza ilifanyika jana usiku katika moja ya kumbi nzuri za Lakairo Hotel ambapo waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali walipata fursa ya kujumuika ktk hili.Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mh.Said Amanzi na washindi
“Nawashukuru sana kwa kuwa mmeisaidia Halmashauri ya jiji la Mwanza kupata heshima katika utumishi sekta mbalimbali na pia kuchangia kuleta amani katika jiji la Mwanza kwa kuwasaidia watendaji wa serikali ngazi zote kufikisha ujumbe wa kile kilichonuwiwa kwa wananchi.” Kauli ya mgeni rasmi.

Kama ilivyo ada kwa kila familia huwa ina kichwa kimoja ambacho kisipoonekana kusanyikoni pana boooa!! basi familia ya habari Mwanza akikosekana kamanda huyu shughuli hainogi. Ni John Maduhu 'Zagamba' ambapo yeye alitupia kitu cha zawadi kwa washindi huku akitanguliza maneno yake 'Ungependa nisemeee!' Ni zawadi gani chekshia picha inayofuata..Kale kawimbo ketu "FU-NGU-A, TU-O-NE yaliyomo"

Sheilla Sezzy wa Mwananchi akifungua zawadi yake aliyo zawadiwa na kamati.

Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi Fredrick Katulanda, Sambamba na kuwapongeza washindi hao kwa kuleta changamoto pia amewaomba MPCT kuona mpango katika zama zijazo Tuzo zitolewe mikoani, tofauti na sasa kwa Tuzo hizo kufanyika jijini Dar es salaam pekee na kisha akasema “Mwanza kuna waandishi wengi wazuri na katika hili tungepata Tuzo nyingi sana zaidi ya hizi ila tatizo wengi sie ni wavivu kushiriki-TUAMKE!”

Mkurugenzi wa UTPC
“Rais hivi majuzi kasema viongozi wa serikali watoe ushirikiano kwa waandishi wa habari ili kusaidia watanzania kujua mafanikio, matatizo yao na mapungufu nao wapate kushiriki au kuchangia katika harakati za utatuzi, Wito kwa mkurugenzi wa jiji la Mwanza aondoe urasimu uliopo wa kutoa habari kwa kutenga siku maalum kwa waandishi kupata habari ili jamii itambue nini kinafanywa na Halmashiauri zake”

Tabasamu la ukweli Sheilla na Asia.

Crew ya Mwananchi Communication Mwanza kutoka kushoto ni Fredrick Katulanda, Sheilla Sezzy na Ray Naluyaga ambaye ni Lake Zone Bureau Chief wa Mwananchi.

Mie in the house'

Marry Misoji na braza Katulanda ndani ya mitegozzZ.

Kuchangamana muhimu.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.