ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, April 22, 2011

SERENGETI FIESTA SOKA BONANZA MAANDALIZI YAMEKAMILIKA MWANZA USHINDWE MWENYEWE.

Katika kuelekea siku husika ya bonanza la Serengeti soka ndani ya jiji la Mwanza leo majira ya asubuhi viongozi wa timu zote nane walifika katika studio za clouds fm Mwanza kwania ya kutangaza usajili wa timu zao sambamba na mikakati waliyoiweka kuibuka washindi kwa michuano hiyo.Pichani ni rais wa Arsenal Mwanza Bw. Arsenal Class akifanya mahojiano na mtangazaji mahiri wa kipindi cha Sports Extra cha Clouds fm, Alex Luambano.

Sambamba na soka kesho mapema subuhi kutakuwa na usaili kuibua wasanii wa filamu na watunzi wa filamu Mwanza, utakao fanyika katika hoteli ya kisasa Isamilo Lodge pichani ni mwigizaji maarufu nchini Jackline Wilper akifafanua jambo kuhusu mchakato mzima.

Rais wa Man U' Mwanza, Fransis Sissamo aka Papaa' amesema timu yake imejipanga kwa ushindi tu! kwani wamejifunza mengi kwa ndugu zao wa Dar es salaam nahawako tayari kurejea makosa.

Mratibu wa usaili Filamu Zamaradi Mketema amewataka washiriki wote waliojiandikisha wajitokeze kwa wingi hiyo kesho jumamosi kwaajili ya kuzinyakuwa Golden Chance zilizopo nikimaanisha kupata dil kuigiza filamu sambamba na mastaa wakubwa.

"Wote wenye vipaji vya kuigiza fikeni Isamilo Lodge kwani hii ni Golden Moment kwani najua ni ndoto ya wengi kwamba siku moja ulitamani kuigiza na kuwa mwigizaji mkubwa basi wakati wa ndoto yako kutimia ndiyo huu" says Hemed.

Timu ya Sports Extra imekamilika kwaajili ya kuripoti matukio yote yatakayojiri ndani ya bonanza la klabu za mashabiki hapa ni Abdul Mohamed akizungumza naye Alex Luambano mbele ya marais wa mashabiki Mwanza ndani ya studio za Clouds 88.1

Hemed, Wolper, G.Sengo na Zamaradi.

Aaaaah Mwanzaaaaa!!

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.