ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, April 28, 2011

MAANDALIZI HARUSI YA KIFALME, UINGEREZA

Mapema leo mjini London kumepambazuka huku kukiwa na shamrashamra za kupindukia na ubize wa ajabu sambamba na matayarisho hayo vikosi vya jeshi la uingereza vilifanya mazoezi ya parade maalum kujiandaa na sherehe za harusi ya mwana wa mfalme.Maharusi.
Nchini Uingereza inshu kubwa inayopamba vinywa vya watu, magazeti na vyombo mbalimbali vya habari ni maandalizi ya harusi ya Kifalme kati ya Kate na William itakayofanyika kesho Aprili 29, 2011.

Organist and Master wa kwaya ya James O'Donnell akiongoza kwaya ya watoto walio mahiri katika uimbaji wa kanisa la Westminster Abbey inayotegemewa kutumika kwenye ibada ya kesho harusini, inatajwa kuwa Prince William ndiye aliyeichagua kwaya hii.

Sherehe hizo za harusi zimepambwa na maandalizi ya kufufuka mtu kwani kila kinachofanyika na kuhusishwa na tukio hilo kimegeuka dili.

Kwa ukakamavu wakipiga kwata nje ya Westminster Abbey ni jeshi la kikosi cha wanamaji.

Farasi.

As the horses walked through the parade ground at Horse Guards, clouds of dust kicked up covering the Welsh Guards, who were lining that part of the procession

Mtihani wa harusi.
Ili kuhakikisha kwamba kila jambo linakwenda kiuhakika zoezi linaendeshwa huku mkaguzi akichukuwa maelezo juu ya nini kibadilishwe kupitia kasoro zinazojitokeza na hata nini kiongezeke katika kuboresha nakuifanya harusi ya kiwango.

Mfanyabiashara John Loughrey (56) amekuwa mfanyabiashara wa kwanza kuweka kambi katika mji wa Westminster Abbey kuuza bidhaa zenye picha na maandiko ya maharusi pamoja na vitambaa na bendera maalum alivyobuni.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.