Aidha wameiomba serikali kuidhibiti mapema hali mbaya ya barabara hiyo kabla mvua zaidi kunyesha hali inayoweza kusababisha zoezi la ukarabati kuwa gumu zaidi, Mpaka sasa maeneo yaliyoathiriwa vibaya na mvua hizo ni pamoja na Katesh na Dareda.
Benki ya Maendeleo ya Afrika imetenga shilingi bilioni 210 kukamilisha ujenzi wa barabara hii ulioanza mwaka 2008 na unaotegemewa kukamilika mwezi wa 8 mwaka huu, benki hiyo imekuwa na utaratibu wa kutoa misaada kugharamia ujenzi wa barabara zetu kwa nia ya kuimarisha ukuaji wa uchumi, kuondoa umaskini na kuboresha hali ya maisha .
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.