
Bw Ghannouchi mwenye umri wa miaka 69, anaonekana kuwa karibu sana na aliyekuwa Rais Zine al-Abidine Ben Ali tangu mwaka 1989, aliyeondoshwa madarakani mwezi uliopita.
Alisema, " Baada ya kutafakari kwa zaidi ya wiki moja, nikaanza kushawishika, na familia yangu iliniunga mkono, na hivyo kuamua kujiuzulu. Si kwamba nakimbia majukumu yangu; nimekuwa nikitimiza wajibu wangu tangu Januari 14." " Siko tayari kuwa mtu anayechukua uamuzi utakaoishia kusababisha vifo." "Kujiuzulu huku kutasaidia Tunisa, mapinduzi pamoja na maendeleo ya siku za usoni za Tunisia." Alisema.
Baada ya saa kadhaa mbadala wa Bw Ghannouchi alitajwa- Beji Caid Essebsi, mwenye umri wa miaka 84, ambaye aliwahi kuwa waziri wa mambo ya nje katika serikali ya marehemu Rais Habib Bourguiba.

Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.