ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, February 18, 2011

KUPITIA 15599 SAIDIA GONGO LA MBOTO KWA HALI NA MALI

ANDIKA NENO maafa KISHA TUMA KWENDA NAMBA 15599Mkurugenzi wa mahusiano wa Vodacom Foundation Mwamvita Makamba pamoja na meneja wa mfuko huo Yassaya Mwakifulefule wakishusha na kukabidhi vyakula mbalimbali wafanyakazi wa Red Cross waliopo katika kiwanja cha Uhuru kwa ajili ya kutoa huduma.

Picha hii ilipigwa kwa mbali asubuhi iliyofuata baada ya mlipuko wa mabomu, inaonyesha moshi ukifuka katika maghala hayo ya silaha eneo la gongo la mboto.

Baadhi ya watoto waliopotezana na wazazi au walezi wao wakiwa wamepewa hifadhi katika uwanja wa Uhuru.

Hapa kulikuwa na biashara ya duka na fundi cherehani.

Endapo usafiri ikatokea ukapatikana na kutokana na mahitaji kuwa makubwa zaidi ya uwezo wa vyombo vyenyewe vya usafiri, basi matumizi yalikuwa kama hivi pichani, muhimu kukimbilia sehemu iliyo salama.

Mabaki ya mabomu yaliyolipuka yakiwa yamekusanywa katika mojawapo ya vitongoji yalikoanguka.

Nyumba hii ilibomoka kutokana na vishindo vya mabomu.

Ili kusaidia ndugu zetu hawa walio katika kipindi kigumu nenda katika ukurasa wa sms (ujumbe mfupi), andika neno MAAFA kisha tuma kwenda 15599 ujumbe huu utakugharimu kiasi cha shilingi 1,000/= tu changia zaidi. Kupitia Vodacom. Na kwa wewe uliyepo Mwanza mkabidhi mchango wako BONGE wa Power Breakfast ndani ya Starmax Hotel iliyopo Kirumba.

@joseph nyaki.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.