Ali Kiba wa Bongo Fleva akitaka kumtoka beki wa Bongo Movie katika mechi iliyochezwa jana jioni katika uwanja wa Taifa jijini Dar.Bongo Fleva waibuka kidedea kwa ushindi wa mabao 2-0 yaliyotiwa kimyani na mshambuliaji H. Baba. Picha kwa hisani ya Othmani Michuzi.
Meya wa Manispaa ya Ilala Jelly Slaa akisalimiana na 'Muuaji' wa Bongo Movie H.Baba.
PICHA ZA VIKOSI KWA HISANI YA JIACHIE>Kikosi kamili cha Bongo Flava Fc.
Kikosi kamili cha Bongo Muvi Fc.
Katika matukio yaliyotengeneza historia kiwanjani hapo moja wapo ni mbwembwe za timu ya bongo Muvi wakiongozwa na kamati yao ya ufundi ikiongozwa na bi Mwenda, Mzee Chilo na wenzake. Dakika jinsi zilivyoendelea kusonga hali ilikuwa mbaya kwao kwani walionekana kukosa raha na kufadhaika mno kwa kichapo walichopokea, kama vile haitoshi mchezaji wao machachari Ben Kinyaiya ilikuwa ni kama kutia chumvi kwenye kidonda kibichi pale alipokosa penati.Dr. Mtitu wa Bongo Movie akikimbia na mpira huku beki wa Bongo Fleva akimfukuzia. Hadi mwisho Bongo Flava 2 Bongo Muvi 0. Mechi hii imefanyika kwa hisani ya kuwachangia watu waliopatwa na maafa/waathiriwa wa milipuko ya mabomu iliyotokea kambi ya Jeshi Gongo la mboto hivi majuzi.
Umoja wa Ulaya Waadhimisha Miaka 50 Tanzania
-
· Siku ya Ulaya 2025 yaadhimisha Miaka 50 ya ushirikiano wa EU na Tanzania
na Miaka 25 ya mahusiano ya EU na AU
· Miongoni mwa wageni rasmi walikuwepo, Mhe...
MHE. SIMBACHAWE AITEMBELEA FAMILIA YA HAYATI MSUYA
-
*Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala
Bora, Mhe. George Simbachawene akizungumza na Familia ya Makamu wa Kwanza
wa Ra...
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.