ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, January 13, 2011

HALMASHAURI YA JIJI LA MWANZA YATOA SIKU 5 KWA WAMACHINGA KUONDOKA KATIKATI YA JIJI.

Halmashauri ya Jiji la Mwanza limetoa siku tano kwa wafanyabiashara ndogondogo maarufu kama wamachinga na mama lishe kuondoka katika maeneo ya katikaki ya jiji kwa vile wamekuwa wakivunja sheria ndongo ya mazingira na usafi namba 312 ya mwaka 2010 na sheria ya Mipango miji na Ujenzi Mijini.Tamko hilo limetolewa juzi na Meya wa Jiji la Mwanza Bw.Josephat Manyerere (Diwani wa Kata ya Nyakato Wilayani Ilemela) kwamba Halmashauri ya Jiji kwa kushirikiana na wakuu wa vilaya za Nyamagana na Ilemela, kikosi cha polisi na vyombo vingine Dola vitaendesha oporesheni kabambe ya kuwaondoa wamachinga hao waliotapakaa kila kona ya jiji wakifanya biashara holela.
Tamko hilo linaonekana kukinzana na lile la ruksa ya kuendelea kufanya biashara toka kwa Mbunge wa Nyamagana Ezekia Wenje (Chadema) alilolitoa siku chache zilizopita wakati akihutubia mkutano wa hadhara wa kulaani tukio la polisi kutumia nguvu kuwatawanya wafuasi wa Chadema Arusha katika mkutano uliofanyika viwanja vya Ngoko’s vilivyopo Kata ya Milongo jijini mwanza.
Meya Manyerere amefafanua kuwa kutokana na hadhi ya Jiji la Mwanza na kusifika kushika nafasi ya kwanza ya usafi kwa miaka mitano mfululizo, likitembelewa na wageni mbalimbali wa kitaifa na kimataifa ili kuilinda hadhi hiyo uongozi hawana budi kuwaondoa wamachinga na mama ntilie ambao wamekuwa kero na kusababisha kuziba barabara za watembea kwa miguu sambamba na kuacha uchafu kila maeneo.
Meya Amewataka wabunge na madiwani wa Jiji la Mwanza kuacha tabia ya kuwapotosha wananchi na badala yake wawe mstari wa mbele kuwaeleza ukweli na kuwaweka tayari kufuata taratibu na sheria zilizopo ili jiji la mwanza liendelee kuwa kioo katika suala la usafi na utunzaji mazingira.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza bw. Wilson Kabwe amewataka wafanyabiashara hao kuzingatia kanuni na sheria kwa kuondoka maeneo yasiyoruhusiwa kufanya biashara na kuelekea kwenye maeneo waliyopangiwa toka awali.

Maeneo yaliyotengwa kwaajili ya wafanyabiashara hao ni Kiloleli, Buzuruga, Kitangili, Nyegezi, Mlango mmoja, Mabatini na kwenye magulio katika maeneo ya Mkuyuni, Igombe, Sabasaba, Nyakato National, Kayenze, Kitangiri, Buhongwa, Mkolani, Igogo, Magomeni Kirumba na Igoma hii ni kwa kufuata siku kama ilivyopangwa na si vinginevyo.

Tupe maoni yako

2 comments:

  1. kweli jiji lisafishwe

    ReplyDelete
  2. Jamani napenda kuuliza huyu meya anawalinda kweli au anawapenda wamachinga?anaonesha anataka kuwarudisha vijijini wakalime hiyo ndiyo sera ya chadema.

    ReplyDelete

Note: Only a member of this blog may post a comment.