Kaimu Mkuu wa shule hiyo ambaye ni Msaidizi mwalimu Mbokela Sahani akipokea msaada huo wa Saruji amesema kwamba viongozi waliopo kwenye Kata hiyo kwa kushirikiana na wazazi waendelee kuisaidia shule hiyo kwakuwa bado inakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo upungufu wa madarasa, Ofisi za walimu (Staff), maktaba na matundu ya vyoo ambayo hayatoshi na yamekwisha jaa.
Mabula amewataka walimu hao kutokubali kutumiwa na baadhi ya watu na wanasiasa kwa lengo la kudhoofisha utoaji wa taaluma na badala yake matatizo yao yapelekwe kwenye vyombo husika ili serikali iyatafutie ufumbuzi wa haraka huku wao wakihakikisha elimu na ufaulishaji wanafunzi katika shule zao ukiboreka kila mwaka na maadili ya watoto yakiwa mazuri.
Tupe maoni yako
Hi! gsengo
ReplyDeletehongera sana na unajitahidi kuwaelimisha,kuwaburudisha na kuwahabarisha watu wa kanda ya ziwa na maeneo ya jirani kwa blog yetu hii kanda ya ziwa.
mimi
Peter kaseko
tuko pamoja