ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, December 6, 2010

MKUTANO WA UWEKEZAJI BONDE LA ZIWA VICTORIA WAANZA JIJINI MWANZA.

Wananchi wanaozunguka eneo la Bonde la Ziwa Victoria wanaendelea kukabiliana na hali ngumu ya maisha na kuishi katika hali ya duni ya maisha, ingawa eneo hilo limejaliwa utajiri wa uoto wa asili na raslimali za kutosha.
MEZA KUU YA KUSANYIKO HILO.
Hayo yamebainishwa leo na Waziri wa Maji Prof. Mark Mwandosya wakati alipokuwa akizungumza kwenye ufunguzi wa kusanyiko la kwanza la uwekezaji katika Bonde la Ziwa Victoria lililofanyika jijini Mwanza na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo wawekezaji kutoka katika nchi za Afrika Mashariki.

WAZIRI MWANDOSYA NA BALOZI MWAPACHU WAKIWASILI ENEO LATUKIO.

MH. MWANDOSYA.
Mwandosya amezitaja changamoto zinazochangia kuwepo kwa hali hiyo ni pamoja na umaskini, migogoro ya kiuchumi, ukosefu wa raslimali watu matumizi mabaya ya vyanzo vya maji , uchafuzi mazingira na ukuaji wa kasi ya ongezeko la watu.

HAFSA MOSSI.
Akifungua mkutano huo, Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Hafsa Mossi amesema kuwa kutokana na raslimali zilizo katika Bonde la Ziwa Victoria, ana imani kuwa wawekezaji wenye sifa watajitokeza kuja kuwekeza kwa lengo la kuwaondolea umaskini wakai wanaozunguka bonde hilo.
Amefafanua kuwa mbali na wananchi kunufaika na ajira, kutokana na uwekezaji huo watapata fursa ya kujipatia maendeleo kwa kujifunza mbinu bora za kisasa za uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara, vyanzo vya nishati ya umeme na usafirishaji na hivyo kuondokana na umaskini wa kipato.

Kusanyiko hilo la kwanza la uwekezaji katika bonde la Ziwa Victoria linalofanyika kwa siku tatu Malaika Hotel Mwanza ambapo jumatano ni hitimisho, Limefanyika likiwa na lengo la kubainisha faida za kiuchumi na kijamii zilizopo bonde la ziwa victoria na kuweza kuvutia wawekezaji kwenda kuwekeza.

WADAU wakijadili haya na yale mara baada ya ufunguzi wa mkutano huo.

The Deputy Prime Minister for Uganda (who seated) posses in a group photo with other East African leaders at Malaika hotel grounds yesterday. From right who seated are the RC for Mara Region Enos Mfuru, The Secretary General for East African Community Ambassador Juma Mwapachu, The Minister for Water Prof Mark Mwandosya, The Deputy Prime Minister for Uganda Hon. Eriya Kategaya, The RC for Mwanza Abbas Kandoro and The Executive Secretary for THE Lake Victoria Basin Commission Dr. Tom Okurut.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.