ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, December 11, 2010

MKUTANO MKUU WA VIJANA VYUO VYA ELIMU YA JUU MWANZA WASHINIKIZA KUANZISHWA KWA BENKI YA VIJANA.

Mgeni rasmi Waziri wa Habari Utamaduni Vijana na Michezo mh. Emmanuel Nchimbi akihutubia ufunguzi wa mkutano huo kwa niaba ya Waziri wa jamhuri ya muungano wa Tanzania, ambapo katika sehemu ya hotuba yake amewataka vijana kujiandaa kikamilifu kwa majukumu yaliyo mbele yao kwani Idara nyingi za serikali na Mashirika binafsi viongozi na watendaji ni vijana.

Waziri Nchimbi akifungua mkutano huo kwa ishara ya kukata utepe.

Waziri Nchimbi akitambulisha Cheti cha Ufunguzi. "Nitafarijika sana Ikiwa wasomi wengi watajihusisha na kuwekeza katika kilimo cha kisasa na ufugaji" Sehemu ya hotuba.

Mkutano huu ni matokeo ya maazimio ya mkutano uliofanyika Dodoma Mwezi juni ambapo uliazimia kufanyika kwa mikutano kama hii ya vijana katika kila kanda ili kujadili changamoto mbalimbali za kimaendeleo.

MA-FOUNDER WA TAYODEFO Kutoka kushoto ni Emmanuel Mgenge, Mgunda Bwere, Patrick Bryoba, Tumaini Kimaro na Christina Benard.

Wataalam wa maendeleo wanaamini kuwa elimu na fedha ni rasilimali muhimu kwa maendeleo hivyo mkutano uliopita wa Dodoma uliazimia pia Uanzishaji wa Benki ya Vijana.

Waziri nchimbi akiagana na wanavyuo mara baada ya kumwakilisha waziri mkuu (Mizengo Pinda) kwenye ufunguzi wa mkutano mkuu wa vijana vyuo vya elimu ya juu uliofanyika katika ukumbi wa BOT CAPRIPOINT, MWANZA.

Kutoka kushoto: Mdau wa TAYODEFO, Mh.NCHIMBI na G.SENGO.

Mgeni rasmi katika picha ya pamoja na Ma-FOUNDER wa TAYODEFO. Vyuo vilivyoshiriki ni pamoja na Chuo kikuu cha mtakatifu Agustin (SAUTI), Chuo kikuu kishiriki cha Afya Bugando (BUCHS) na Chuo cha Elimu ya biashara (CBE) kampasi ya Mwanza. Mashirika mbalimbali yanayojihusisha na masuala ya vijana kupigana vita juu ya UKIMWI na Madawa ya kulevya nayo ndani.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.