ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, December 9, 2025

MECHI ZA LEO UEFA NI PRESHA TUPU....


Italia kutakuwa na mechi ya kukata Inter Milan vs Liverpool ambao hivi karibuni wamekuwa na matokeo ambayo hayaridhishi kabisa kwani kwenye mechi 13 amabzo amecheza ameshinda 3 pekee. Mara nyingi hawa wawili kukutana ilikuwa kwenye fainali na Jogoo wa Anfield alipoteza. 

Vijana wa Diego Simeone, Atletico Madrid watakuwa ugenini kukiwasha dhidi ya PSV kutoka kule Uholanzi lakini pia imeweza kupata matokeo dhidi ya timu kubwa kwenye michuano hii. 

AS Monaco atakuwa nyumbani kupepetana dhidi ya Galatasaray ambao walipoteza mechi yao iliyopita wakiwa nyumbani. Mwenyeji yeye alitoa sare, hivyo pointi 3 ni muhimu kwa timu zote siku ya leo. 

Marseille yeye atakuwa kibaruani kumenyana vikali dhidi ya Union St.Gilloise ambao wanahitaji ushindi siku ya leo ili wasogee mbele kwenye michuano hii. Tofauti ya pointi kati yao hadi sasa ni hakuna kwani wote wana pointi sawa. 


Bayern Munich yeye atakipiga dhidi ya Sporting CP ambapo mpaka sasa kwenye mechi 8 ambazo amecheza amekusanya pointi 10 huku vijana wa Kompany wao wakichukua pointi 12. Mwenyeji ametoka kupoteza huku mgeni yeye akishinda. 

Kwa upande wa Chelsea wao watakuwa ugenini kukipiga dhidi ya Atalanta baada ya mechi iliyopita kushinda, halikadhalika kwa wenyeji nao walishinda. 


Vijana wa Hans Flick, FC Barcelona watakuwa nyumbani kusaka ushindi dhidi ya Eintracht Frankfurt ambao wana pointi 4 pekee hadi sasa huku Wacatalunya wao wakiwa na pointi 7. Barca wanahitaji ushindi kwa namna yoyote ile ili wajiweke kwenye nafasi nzuri ya michuano hii.  

Tottenham  Spurs atakuwa kibaruani kukipiga dhidi ya Slavia Prague ambao kwenye mechi 5 wameambulia pointi 3 pekee. Huku wenyeji wao wakiwa na pointi 8 hadi sasa. 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment