ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, August 21, 2025

"MUSTAKABALI WA TAIFA LETU HUPIMWA KUPITIA CHAGUZI TUNAZOFANYA" DC MAKILAGI

 


“𝙈𝙪𝙨𝙩𝙖𝙠𝙖𝙗𝙖𝙡𝙞 𝙬𝙖 𝙏𝙖𝙞𝙛𝙖 𝙡𝙚𝙩𝙪 𝙝𝙪𝙥𝙞𝙢𝙬𝙖 𝙠𝙪𝙥𝙞𝙩𝙞𝙖 𝙘𝙝𝙖𝙜𝙪𝙯𝙞 𝙩𝙪𝙣𝙖𝙯𝙤𝙛𝙖𝙣𝙮𝙖.”

.
Nikiwa kama kiongozi mwanamke, nachukua nafasi hii kuhamasisha wanawake wote nchini kujitokeza kwa wingi kushiriki katika mchakato wa uchaguzi.

Tunapozungumzia mustakabali wa Tanzania, tunazungumzia uongozi bora—uongozi unaojali usawa wa kijinsia na unaomgusa mwanamke katika kila nyanja ya maisha.

Ni wajibu wa kila mwanamke kushiriki kikamilifu kwenye uchaguzi. Tuna mfano hai na wa kuigwa, Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye kupitia nafasi yake ameonesha kuwa mwanamke anaweza, ana haki na ana mchango mkubwa katika maendeleo ya taifa.

Jitokeze. Shiriki. Chagua kwa uelewa. Tanzania ni yetu sote. — Mhe. Amina Makilagi, Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Kupitia kipindi cha Kazi na Ngoma
.
.
#KaziNaNgoma
@jembefmtz

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment