![]() |
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan. |
Rais Samia Suluhu Hassan, atakuwa mgeni rasmi katika sherehe za uapisho wa Rais mteule wa kwanza mwanamke wa Jamhuri ya Namibia, Netumbo Nandi-Ndaitwah, zitakazofanyika leo Machi 21,2025.
Rais Samia Suluhu Hassan, atakuwa mgeni rasmi katika sherehe za uapisho wa Rais mteule wa kwanza mwanamke wa Jamhuri ya Namibia, Netumbo Nandi-Ndaitwah, zitakazofanyika leo Machi 21,2025.
Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa Mei 20,2025 na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Rais. Samia atahutubia kwenye sherehe hizo za uapisho zitakazofanyika sambamba na Maadhimisho ya Miaka 35 ya Uhuru wa Namibia.
Aidha, taarifa hiyo imefafanua kuwa mahusiano baina ya Tanzania na Namibia ni ya kidugu na kihistoria ambayo yaliasisiwa na Hayati Julius Nyerere na Hayati Sam Nujoma kipindi cha harakati za ukombozi wa nchi za Kusini mwa bara la Afrika.
“Mahusiano haya yameendelea kukuzwa na kulelewa na Viongozi wote wakuu waliowafuatia katika nyanja mbali mbali,”imefafanua taarifa hiyo.
Kadhalika, mbali na kuhudhuria sherehe hizo Rais Samia atapata fursa ya kusalimiana na mwenyeji wake na kufanya mazungumzo ya kukuza na kuimarisha mahusiano.
“Kwa mara ya kwanza Namibia itapata Rais Mwanamke hivyo kufanya idadi ya Marais Wanawake barani Afrika kuwa wawili akiwemo Rais Samia,”imefafanua.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.