Leo Januari 30, 2025 mkoani Geita, maelfu ya waombolezaji wamejitokeza kuaga miili ya wanafunzi saba wa Shule ya Sekondari Businda iliyopo wilayani Bukombe waliofariki kwa kupigwa na radi mnamo tarehe 27 januari, 2025.
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Bukombe, Mhe. Dkt. Doto Biteko ameongoza shughuli za kuaga na kukabidhi ubani kwa wafiwa huku akiwataka kuwa wavumilivu hasa kipindi hiki cha majonzi.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.