ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, May 15, 2024

POLISI PWANI YAONYA BODABODA WANAOVAMIA MISAFARA YA VIONGOZI.

IMEANDALIWA NA VICTOR MASANGU/PWANI NA KUSOMWA NA ALBERT G. SENGO

JESHI la Polisi Mkoa wa  Pwani limewaonya  vikali baadhi ya  madereva wa Bodaboda kuacha kabisa tabia kuingilia misafara ya viongozi waandamizi na badala yake wanapaswa kuiheshumu pindi inapopita ili kuweza kuepuka ajali ambazo zinaweza kupelekea watu kujeruhiwa vibaya na kupoteza maisha.


Onyo hilo  limetolewa na Kamanda wa Polisi mkoani Pwani  wakati Jeshi la Polisi  kwa kushirikiana na Kampuni ya Pyriamid Oil walipotoa Elimu ya usalama barabarani sambamba na  uzinduzi rasmi  wa kituo ha mafuta  kilichopo eneo la kwa Mbonde  mkoani Pwani

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.