ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, February 28, 2024

WANANCHI KATA YA MSANGANI KUFANYA UCHAGUZI WA UDIWANI MACHI 20


NA VICTOR MASANGU,KIBAHA

Uchaguzi wa kujaza nafasi iliyoachwa wazi  ya udiwani  katika kata ya Msangani iliyopo Halmashauri ya mji Kibaha mkoani Pwani unatarajiwa kufanyika machi 20 mwaka huu.


Akizungumza na mwandiishi wa habari hizi ofisini kwake   Katibu wa chama cha mapinduzi  (CCM) Wilaya ya Kibaha Mjini Issack Kalleiya alisema kwamba katika kuelekea uchaguzi huo tayari wameshapokea majina matatu ya wagombea.


Katibu huyo alifafanua kwamba kamati ya siasa ya Wilaya imeshapokea majina matatu ya wagombea wa nafasi hiyo ya udiwani kutoka kamati ya siasa ya kata ya msangani.


Aidha Katibu huyo alisema kwamba baada ya kupokea majina hayo kamati ya siasa ya Wilaya imeyapitia na kuamua kuyapitisha yote kwa pamoja na kuyawasilisha katika kamati ya siasa ya Mkoa ili yaweze kupitiwa.


Pia aliongeza kuwa majina ambayo yamepitishwa kwa ajili ya kugombea nafasi hiyo ya  udiwani ni pamoja na Gunze Chongela,Khamis Mwande pamoja na Tatu Ashura.

Kadhalika alisema kwamba baada ya hapo  majina hayo matatu yaliyopendekezwa kupelekwa katika kamati ya siasa ya Mkoa ili  kuweza kuteuliwa na   kwenda   kugombea katika  nafasi hiyo ya udiwani.


Katibu huyo aliwaomba viongozi wote na  wanachama wote wa kata ya Msangani kuungana kwa pamoja na kuvunja makundi na kumpa ushirikiano mtu ambaye atachaguliwa kugombea nafasi hiyo.

Alisema kwamba kwa kuwa zoezi la mchakato mzima wa kuwachagua wagombea hao lilianzia kwao hivyo wanapaswa kuhakikisha wanashiriki kikamilifu katika uchaguzi huo na kuwa kitu kimoja kwa maslahi ya chama.


 Katibu huyo alitoa wito kwa wanachama hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi huo wa udiwani kuweka tofauti zao pembeni na kujitokeza kwa wingi pamoja na wananchi katika uchaguzi huo ambao utafanyika Machi 20 mwaka  huu.


Hivi karibuni aliyekuwa diwani wa kata ya Msangani kupitia tiketi  ya chama cha mapinduzi Leonard Mlowe alifariki dunia na hivyo kupelekea nafasi yake kubaki wazi.


                   MWISHO

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.