ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, January 14, 2024

RC PWANI AZINDUA RASMI MRADI MKUBWA WA KILIMO CHA PAMBA RUFIJI

 VICTOR MASANGU PWANI 

 Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaj Abubakari Kunenge  amezindua  Mradi wa kilimo cha Pamba Wilayani  Rufiji utakaotekelezwa na Kampuni ya Rufiji Cotton Ltd ambapo uzinduzi huo umeambatana na kupokea matrekta na pikipiki zitazotumika kwenye mradi huo.

Akizungumza na Wanachi wa Rufiji wakati wa hafla hiyo, Mhe Kunenge amewapongeza wawekezaji  hao kutoka India kwa uwekezaji huo amesema hana shaka na mwekezaji  huyo kwa sababu ni mzoefu kwenye sekta ya Pamba.



Kunenge amesema  kuwa  kwenye historia Pamba ilianza kulimwa Nchini  kwa mara ya kwanza wilayani Rufiji mwaka 1964 Amesema kuwa  Serikali ipo tayari kuumpa ushirikiano  mwekezaji na  kimtaka mwekezaji Afanye  yote aliyoahidi.

 Ameeleza Kupitia uwekezaji huo vijana watapata ajira, Kodi kwa serikali na ujuzi. Ameeleza kuwa  kwenye kipaumbele chake kwa Mkoa wa Pwani Kilimo ni kipaumbele na bado hakijafanya vizuri. 

Pia amepongeza wilaya ya Rufiji kwa  kuendelea  kuwapokea wawekezaji kwa sasa wilaya hiyo ina wawekezaji wakubwa wa Kilimo cha Sukari, na Kilimo cha Pamba. Kunenge amewataka wakazi wa Rufiji kutumia fursa hizi walizopata. Amewapongeza  wakazi wa chumbi kwa kuwezesha uwekezaji huo.
Naye Mkurugenzi  Mkuu wa Bodi ya Pamba  Bw. Wille Mtunga  ameeleza kuwa ziara ya India ya Mhe Rais  Dkt. Samia Suluhu Hassan imezaa matunda na leo tunazindua mradi wa Pamba Rufiji.  

 Alisema  kuwa  ili kuwa na kilimo bora wameleta timu ya  ushindi ambao ni maafisa ugani 24  watakao hudumu kwenye vijiji hivyo  24. ameeleza kuwa  Mpaka sasa wamesajili wakulima wenye jumla ya  Hekari 3012 wilayani Rufiji.

Naye Balozi wa  zao la Pamba  Nchini Mhe Aggrey Mwanri, ametuma Salaam kwa Mhe Rais  Dkt Samia za pongezi kwa kuvutia uwekezaji katika sekta ya Pamba. 

Ameeleza kuwa kazi yake  kama balozi ni kufanya pamba ipendeke kwa wananchi wote. Ameeleza wamechukua takwimu za wananchi wote wa Rufiji waliotayari kulima Pamba. 

Ameeleza kuwa Kilo zinazozalishwa  wilayani Rufiji ni laki moja na kiwanda  kitakacho jengwa kitahitahi kilo laki tano. Ameeleza  kuwa Halmshauri hiyo ikilima pamba vizur itapata ruzuku amehamasisha vijana wote kulima pamba na wale maafisa ugan 24 walioajiriwa kuhakikisha wanafanya kazi iliyokusudiwa.

Naye Mkurugenzi  Mkuu wa Kiwanda cha Rufiji Cotton Ltd  Bw Hassan Kinje   ameeleza  kuwa wamekuja kuwekeza Rufiji kwa sababu ya Mazingira mazuri ya uwekezaji, ameeleza kuwa wamekuja kulima Rufiji na si Kununua Pamba. Ameeleza kuwa kampuni hiyo itatoa uwezeshaji wa huduma bure ya  matrekta kwa ajili ya kilimo. 
Aidha wameajiri maafisa ugani 24  na kutoa pikipiki ambazo zitatumika kutoa  elimu kwa wakulima. Ameeleza kuwa  wanategemea kujenga kiwanda cha kuchambua Pamba, kiwanda vya nguo. Wamepongeza ushirikiano mkubwa walioupata kutoka katika uongozi  wa Mkoa katika kufanikisha uwekezaji huo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.