ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, November 6, 2023

RAIS SAMIA ATOA ML 252 UKARABATI WA DARAJA LA MTO MPIJI

 VICTOR MASANGU, PWANI


Wananchi wa Kata ya Pangani katika halmashauri ya mji Kibaha ambao walikuwa wanakabiliwa na changamoto ya adha kubwa ya kuvuka  katika daraja la mto Mpiji wanakabiliwa kuondokana na kero hiyo baada ya serikali kutoa fedha ambazo zitasaidia katika  ukarabati  wa miundombinu na kuzuia kingo kubomoka.


Hayo yamebainishwa na  Meneja wa Tarura Wilaya ya Kibaha Samwelu Ndoveni akisema  kwamba tayari wamepokea kiasi cha shilingi milioni 252 kwa ajili ya kufanya matengenezo haraka zaidi  katika daraja hilo la Pangani.

INSERT..1 TV SAMWELI NDOVENI MENEJA WA TARURA WILAYA YA KIBAHA

Naye Mbunge wa Jimbo la Kibaha mji ambaye amefika katika daraja hilo kujionea amempongeza Rais wa awamu ya sita Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kukubali kutoa fedha hizo ambazo zitasaidia kuboresha  daraja hilo liweze kupitika kwa urahisi hasa katika kipindi hiki cha mvua.


INSERT..2 TV SILVESTRY KOKA MBUNGE JIMBO LA KIBAHA MJI.

Mkuu wa Wilaya ya Kibaha amesema kwamba wananchi wa kata ya Pangani ambao wanatumia daraja hilo wamekuwa wakipata adha kubwa hasa katika kipindi cha mvua na kwamba fedha hizo zitakwenda kutumika kwa manufaa ya wananchi.

INSERT..3TV NIKSON SAIMONI MKUU WA WILAYA YA KIBAHA.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.