ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, June 6, 2023

VODACOM MWANZA YASHIRIKI SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI KWA KUFANYA USAFI MAENEO SUGU NA KOROFI

 NA ALBERT G.SENGO/MWANZA

Siku ya Mazingira Duniani  inayoadhimishwa kila mwaka tarehe 5 mwezi wa Juni, huleta pamoja mamilioni ya watu kote duniani na kuwashirikisha kwenye jitihada za kutunza na kuboresha Dunia. Mwaka huu ni maadhimisho ya miaka 50 ya Siku ya Mazingira Duniani. Siku ya Mazingira Duniani ni jukwaa la kimataifa la kuchochea mabadiliko chanya. Watu kutoka kwa zaidi ya nchi 150 hushiriki katika siku hii ya kimataifa ya Umoja wa Mataifa, ambayo inasherehekea hatua za kushughulikia mazingira na uwezo wa serikali, mashirika ya biashara na watu binafsi kuunda ulimwengu endelevu zaidi. Hafla hii imekuwa likisimamiwa na Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP) tangu kuanzishwa kwake katika mwaka 1973. HISTORIA Siku ya Mazingira Duniani huangazia changamoto kuu za mazingira tunazokumbana nazo kwa sasa duniani. Siku hii ya kimataifa ya umoja wa mataifa imepanuka na kuwa jukwaa kuu la kimataifa la kuhamasisha kuhusu mazingira huku mamilioni ya watu wakishiriki ili kutunza mazingira. Kutoka jijini Mwanza Vodacom imeshiriki shughuli za usafi kwenye maeneo sugu na korofi katikati ya jiji la hilo

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.