ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, May 16, 2023

MAMA ALIYENASWA KWENYE VIDEO AKIMLISHA MTOTO WA KAMBI KINYESI AKAMATWA

 


Mwanamke mwenye umri wa miaka 26, ambaye alinaswa kwenye video akimlisha mtoto wake wa kambo mwenye umri wa miaka 4, kinyesi amekamatwa

 

Kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na polisi nchini Uganda Jumatatu, Mei 15, mwanamke huyo anazuiliwa katika Kituo cha Polisi cha Jinja ambapo kesi ya kuteswa na unyanyasaji wa watoto ilifunguliwa dhidi yake.

 

Video hiyo ambayo tarehe yake ya kurekodiwa haijulikani, inamuonyesha mwanamke huyo ambaye polisi wamemtambua kwa jina la Esther Nabirye, akimlazimisha mtoto huyo kula kinyesi chake baada ya kudaiwa kujisaidia haja kubwa kwenye sebule.

 

Msemaji wa polisi, Fred Enanga alitaja vitendo vya Nabirye kuwa vya kinyama na visivyo vya kibinadamu.

 

Polisi walisema mvulana huyo atapelekwa kwenye makazi ya dharura ya watoto

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.