ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, March 10, 2023

VIJANA MWANZA WAONGOZA KUTAKA KUUZA FIGO 'WAKALE BATA'

 NA ALBERT G. SENGO/MWANZA

VIJANA jijini #Mwanza wametajwa kuongoza katika biashara ya kuuza figo kutokana na hali ya ugumu wa maisha. Hayo yamebainishwa na Dr. Bingwa na mbobezi wa magonjwa ya figo katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya #Bugando Said Kanenda katika maadhimisho ya Siku ya Figo Duniani hii leo ambapo amesema wakazi saba kati ya mia moja wa vijijini wanasumbuliwa na ugonjwa figo. Kutokana na uwepo wa takwimu hizo Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Bugando imesema wagonjwa 150 wanapatiwa matibabu katika kliniki ya magonjwa ya figo kila wiki sawa na wagonjwa 600 kwa mwezi ambao hawajaanza atibabu ya kutoa taka mwili.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.