ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, March 16, 2023

KAMA KUNA KAMPUNI YA BIMA INAKUZUNGUSHA HAITAKI KUKULIPA HILI HAPA SULUHISHO.

 NA ALBERT G.SENGO/MWANZA

Zipo changamoto nyingi ambazo jamii imekuwa ikikumbana nazo wakati wa kudai fidia za bima mbalimbali, iwe chombo cha moto cha usafiri, bima ya nyumba, kampuni, bima ya afya au hata pengine pale mtu kutoka ndani ya jamii anapotumikia kazi au ajira yake kwa uaminifu na ikafika wakati wa ulipwaji kukazuka changamoto katika udai wa fidia.

Kupitia maonesho ya WIKI YA NENDA KWA USALAMA BARABARANI iliyofanyika katika viwanja vya Furahisha jijini Mwanza, Jembe Fm inadhuru katika banda la Ofisi ya Msuluhishi wa Migogoro ya Bima ambapo inapata maelezo kwa kina. Sasa basi kama unachangamoto ya kupunjwa fidia, kutoridhika na kiwango cha fidia, kucheleweshewa malipo, kukataliwa madai yote, huu ni wasaa wako wa utatuzi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.