ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, February 3, 2023

"WANASIASA SOMENI KWANZA MIKATABA YA MIRADI KABLA YA KUFANYA MAAMUZI ILI KUIEPUSHA HASARA SERIKALI"

 NA ALBERT G.SENGO/MWANZA

Mafunzo kwa Wakandarasi na wadau wa Sheria kwa taasisi za Serikali juu ya usimamizi wa mikataba ya ujenzi ili kuboresha utendaji na kusimamia miradi imalizike kwa wakati pamoja na kuiepusha Serikali na hasara kwa kesi zinazozuilika yaliyofanyika kwa muda wa siku 5 yamemalizika leo jijini Mwanza. Mafunzo hayo yaliandaliwa na Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) ambalo tangu kuanzishwa kwake moja ya majukumu yake katika sheria yake ni kusimamia ukuaji wa sekta ya ujenzi nchini ili kwenda sambamba na maendeleo na ushindani wa kimataifa. Majukumu mengine ni pamoja na Kuishauri Serikali kuhusu masuala yanayohusu sekta ya ujenzi na kutayarisha mapendekezo, maelekezo na utekelezaji wake; Kutoa ushauri wa kiufundi kwa wadau wa sekta ya ujenzi, Kukuza na kuratibu mafunzo bora kwa watu wanaojihusisha au watakaojihusishana sekta ya ujenzi na Kukuza, kuendesha na kuratibu utafiti katika masuala yanayohusiana na sekta ya ujenzi. Jeh yapi yamejiri ndani ya mafunzo hayo........

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.