ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, January 9, 2023

MBRAZIL WA SIMBA AMEANZA TAMBO.

 

KOCHA Mkuu wa Simba, Roberto Oliviera raia wa Brazil ameweka wazi kuwa kwa namna ambavyo ameanza kazi na wachezaji wa timu hiyo amefurahishwa na uwezo wao.

Kocha huyo raia wa Brazil amepewa mikoba ya Zoran Maki aliyevunja mkataba na timu hiyo mwanzoni mwa msimu wa 2022/23.

Nchini Dubai Simba imeweka kambi yake ambayo itachukua siku saba tayari wameanza mazoezi kwa ajili ya kuandaa kikosi hicho kilichotoka kuvuliwa ubingwa wa Kombe la Mapinduzi.

Kocha huyo amesema:”Nimeona wachezaji wakijituma na inaonyesha kabisa wana vipaji kwenye uchezaji pamoja na kutimiza majukumu yao hivyo nina amini tutakuwa imara kwenye mbinu,”.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.