ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, June 4, 2022

WAPI PAKUPATA UNAFUU KWA WATOTO WAFANYAKAZI MAJUMBANI?


WAPI PA KUPATA UNAFUU ? Kesi au masuala yote yanayohusu watoto yanahusu pia jamii yote, jeshi la polisi, madaktari, serikali za mitaa, na maafi sa wa ustawi wa jamii katika kila serikali za mitaa.

 Mahakama ya watoto itahusika katika mambo yote yanayohusu watoto. Ikiwa mtoto amefanyiwa vitendo vilivyotajwa hapo juu, wazazi/mwanajamii anaweza kutoa taarifa katika serikali ya mtaa, ambayo kwa kushirikiana na afi sa ustawi wa jamii, wana wajibu wa kufuatilia ulinzi na ustawi wa mtoto huyo aliyedhurika. 

Ikihitajika kwenda mahakamani, afi sa ustawi ana wajibu wa kupeleka maombi mahakamani juu ya nafuu ya au ulinzi wa mtoto huyo. 

 Angalizo: Serikali ya mtaa ina wajibu kutokana na sheria ya mtoto, kuwatafutia na kuwapa hifadhi watoto ambao wametelekezwa au kukosa makazi.

Pia ina wajibu, kwa kushirikiana na afi sa ustawi wa jamii, kuwatafuta wazazi waliotelekeza watoto na kuwarudisha, au kutoa amri ya matunzo. Shirika la Kutetea Haki za Watoto wafanyakazi Nyumbani la Nuru Organisation.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.