ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, April 13, 2022

ZAIDI YA WANAJESHI 1,000 WA UKRANE WAJISALIMISHA HUKO MARIUPOL - URUSI

 

Urusi inadai wanajeshi 1,026 wa Ukraine wameweka silaha chini katika mji unaozingirwa wa Mariupol.


Bandari ya kusini imekuwa ikishambuliwa kwa wiki kadhaa na inaaminika kuwa inaelekea kuanguka mikononi mwa Urusi.


Kikosi hicho, cha 36 cha Marine Brigade, lilisemekana kujisalimisha karibu na kiwanda cha kutengeneza mabati na vyuma cha Ilyich Iron and Steel.


Msemaji wa wizara ya ulinzi ya Ukraine Oleksandr Motuzyanyk amesema kwamba hajapokea taarifa kuhusu ripoti hizo.


Mapema wiki hii, naibu meya wa Mariupol alitaja kuwa "feki"chapisho la Facebook lililodai kuwa wanajeshi wa kikosi hicho walikuwa wameishiwa na risasi na kwamba wamekosa uungwaji mkono.


Huku hayo yakijiri familia ya Muingereza anayepigana nchini Ukraine imesema amewaambia kwamba atalazimika kujisalimisha kwa vikosi vya Urusi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.