ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, April 6, 2022

MFUMUKO WA BEI WAFIKIA ASILIMIA 3.7

 


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema katika mwaka 2021, mfumuko wa bei ulikua kwa wastani wa asilimia 3.7 ikilinganishwa na wastani wa asilimia 3.3 mwaka 2020.


Majaliwa amezungumza hayo leo Jumatano Aprili 6, 2022 katika hotuba ya Maombi ya Makadilio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2022/23 katika mkutano wa bunge Jijini Dodoma.


Waziri Mkuu amesema kuongezeka kwa mfumuko wa bei kulichangiwa na sababu mbalimbali ikiwemo atahari za Uviko-19, kuongezeka kwa gharama za uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa bidhaa na huduma, kupungua kwa upatikanaji wa mazao ya chakula katika baadhi ya masoko ya ndani kutokana na mabadiliko ya tabianchi.


Amesema mfumuko huo ulikuwa ndani ya lengo la muda wa kati ya asilimia 3 – 5 ambapo wigo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki usiozidi asilimia 8 na ndani ya wigo 17 wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika wa kati ya asilimia 3 - 7.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.