ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, March 27, 2022

RAIS JOE BIDEN AKOSOA UTAWALA WA PUTIN NCHINI URUSI

 


Rais wa Marekani Joe Biden amesema rais wa Urusi Vladimir Putin hawezi kusalia mamlakani baada ya kuivamia Ukraine huku akiyaonya majeshi Urusi kutojaribu kusogeleea eneo la jumuiya ya kujihami ya NATO. 


Biden amesisitiza katika hitimisho la ziara yake ya siku mbili nchini Poland kwamba Putin hawezi kubakia madarakani na kuongeza kuwa vita vyake dhidi ya Ukraine ni mkakati wa Moscow ulioshindwa.


Matamshi yake makali na yasiyo ya kawaida hata hivyo yalidhoofishwa na ikulu ya Washington ambayo ilisema hakumaanisha kutoa mwito wa serikali ya Putin kuondolewa madarakani. Na baada ya ikulu ya Kremlin kuulizwa kuhusu matamshi hayo ya Biden msemaji alisema tu kwamba huo sio uamuzi wa Biden kwa kuwa rais wa Urusi alichaguliwa na raia wa Urusi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.