ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, March 24, 2022

HRW YAITAKA ETHIOPIA KUCHUNGUZA SHAMBULIO LA ANGA DHIDI YA SHULE.

 


Shirika la kimataifa la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch, limeitolea mwito Ethiopia leo, kufanya uchunguzi wa shambulio la anga lililofanywa dhidi ya shule moja katika jimbo la Tigray ambalo liliuwa watu kadhaa. 

Shambulio hilo huenda likawa ni uhalifu wa kivita. Shirika hilo limesema mabomu matatu yalirushwa Januari 7 dhidi ya shule iliyokuwa ikiwahifadhi Watigrinya katika mji wa Dedebit na kuwaua kiasi watu 57 na kuwajeruhi wengine zaidi ya 42. 

Human Rights Watch limesema serikali ya Ethiopia inapaswa kufanya uchunguzi wa kina na usioegemea upande kuhusu tukio hilo ambalo huenda lilikuwa uhalifu wa kivita na kuwachukulia hatua zinazostahiki waliohusika. 

Waliouwawa kwenye shambulio hilo walikuwa zaidi wazee, wanawake na watoto waliokuwa wakilala kwenye mahema yaliyotengenezwa kwa plastiki na shirika hilo limesema hakukuwa na ushahidi wa kuonesha walikuweko wanajeshi waliolengwa katika tukio hilo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.