ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, February 2, 2020

POLISI YATHIBITISHA VIFO VYA WATU 20 KWENYE IBADA MKOANI KILIMANJARO/ WAZIRI WA MAMBO YA NDANI NAYE AZUNGUMZA


Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi George Simbachawene amesema Nabii na Mtume, Boniphace Mwamposa alikaidi taratibu za kibali kilichomtaka afanye huduma mpaka saa 12 jioni, huduma aliyoitoa hadi saa 2 usiku na kuwaamuru waumini wakanyage mafuta kabla ya maafa hayo kutokea.

Simbachawene ameyasema hayo Jijini Dodoma leo Jumapili Februari 2, 2020 wakati akizungumza na waandishi wa habari na kusema baada ya Mwamposa kuona maafa hayo yametokea, alitoroka ili kukwepa polisi na kurudi jijini Dar es Salaam usiku huohuo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.