ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, November 13, 2019

Chama cha CUF nacho chajitoa katika uchaguzi wa serikali za mitaa nchini Tanzania

Habari kutoka Dar es Salaam nchini Tanzania zinasema kuwa Chama cha Wananchi (CUF)  hatimaye kimejitoa katika uchaguzi wa serikali za mitaa uliopangwa kufanyika Novemba 24 mwaka huu.
Kimesema kuwa  kimejitoa katika uchaguzi wa serikali za mitaa kutokana na kutoridhishwa na mwenendo wa mchakato huo ikiwa ni pamoja na kuenguliwa asilimia 90 ya wagombea wake. 
Msimamo huo umetangazwa leo Jumanne na Mwenyekiti wa chama hicho Profesa Ibrahim Lipumba wakati akitoa maazimio ya kikao cha baraza kuu la uongozi la CUF. CUF kinakuwa chama cha siasa cha sita kujitoa katika uchaguzi wa Serikali za mitaa nchini Tanzania baada ya Chadema, ACT- Wazalendo, NCCR –Mageuzi, UPDP na Chauma.
Katika maelezo yake Profesa Lipumba amesema kuwa baraza hilo limetafakari kwa kina na kuona hakuna umuhimu kushiriki uchaguzi baada ya hoja zao tatu walizoziwasilisha serikalini kutofanyiwa kazi. "Uchaguzi unatakiwa uwe huru na haki lakini serikali imeshindwa kuonyesha hata chembe ya haki. Asilimia 90 ya wagombea wetu wameondolewa tumebaki na asilimia nne tu", amesisitiza Lipumba. Ameongeza kuwa katika mazingira hayo ni wazi kuwa CUF imeondolewa kwa sababu haiwezi kushiriki bila wagombea.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.