ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, October 6, 2019

PICHA: WACHEZAJI WA NGORONGORO HEROES WAWASILI SALAMA NCHINIBAADA YA KUNYAKUA UBINGWA.







TIMU ya Taifa ya Tanzania chini ya umri wa miaka 20 'Ngorongoro Heroes' leo imerejea ikiwa na ubingwa na kupokelewa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Harrison Mwakyembe.

Ngorongoro imetwaa ubingwa huo jana kwenye michuano hiyo iliyofanyika nchini Uganda kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Kenya.

Tanzania haikupoteza mchezo hata mmoja kwenye michuano hiyo ililazimisha sare ilipocheza na Kenya kwenye hatua ya makundi.

Ilikuwa kundi B lenye timu nyingine za Zanzibar, Ethiopia, Kenya.


Mabingwa wa CECAFA U20 Timu ya Vijana U20 Tanzania Bara wamewasili salama na kupokelewa na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.