ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, October 21, 2019

AKINABABA NA FEDHA ZA MASHARTI KISA CHA KUWATESA WENGI


Jinsi ya kiume imetajwa kuwa ni moja kati ya watendaji wakubwa wa vitendo vingi vya ukatili dhidi ya Mwanamke na Mtoto katika jamii ambavyo vimekuwa vikiathiri malezi ya watoto na ustawi wa familia.

Hayo yameainishwa na wazazi pamoja na wanafunzi katika mdahalo wa kutoa elimu kwa jamii kupinga aina zote za ukatili wa kijinsia wilayani Misungwi mkoani Mwanza kufuatia swali la majadiliano liliulizwa kwa wanafunzi na aliyekuwa mwendesha mada Mkurugenzi wa Shirika la kutetea haki za wanawake na watoto la KIVULINI Yassin Ally  kwamba "Kama ikitokea Mungu akakupa nafasi uchague nani abaki duniani kati ya mama au baba utapenda nani abaki?" Nayo majibu mengi yakaelekea kumtetea mama.

Hatua hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa awamu ya pili ya mpango mkakati wa kitaifa wa kupambana na ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto (MTAKUWWA) uliozinduliwa na Halmashauri ya Wilaya Misungwi kwa kushirikiana na Shirika la KIVULINI katika Kata ya Koromije, Oktoba 16, 201 na baadae kuendelea katika Kata zingine.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.