ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, September 26, 2019

VIDEO: MWILI WA NELSON MABEYO ULIVYOPOKEWA MWANZA - MAZISHI LEO ALHAMIS 26 SEPT 2019

 Hatimaye Mwili wa  rubani, marehemu Nelson Mabeyo umewasili jijini Mwanza tayari kuelekea kijiji cha Masanzakona wilayani Busega mkoani Simiyu kwaajili ya mazishi.

Nelson ambaye alikuwa rubani wa ndege ya Kampuni ya Auric air yenye namba 5H-AAM alipata ajali katika uwanja wa Serengeti akiwa na Nelson Orutu ambaye ni rubani mwanafunzi na wote kwa pamoja walifariki dunia papo hapo.


Miili ya wawili hao akiwamo wa rubani huyo ambaye ni mtoto wa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini Tanzania (CDF), Jenerali Venance Mabeyo ilihifadhiwa katika Zahanati ya Soronera kisha baadaye kusafirishwa hadi jijini Dar es salaam, ambapo jana Jumatano uliwasili jijini Mwanza na kuelekea kijiji cha Masanzakona wilayani Busega mkoani Simiyiu kwaajili ya mazishi yatakayofanyika leo Alhamisi ya tarehe 26 Septemba 2019.




Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.