ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, September 25, 2019

KUTANA NA HISENSE BIDHAA ZENYE WARRANTY MIAKA MITATU - ZATINGA KANDA YA ZIWA.


Bidhaa za HiSENSE tayari zimeshatinga nchini Tanzania na katika maonesho ya biashara ya madini yaliyofanyika mkoani Geita imepata kushiriki. Hii ni Kampuni iliyopata mafanikio barani Afrika kutokana na kutengeneza bidhaa zenye chapa yake yenyewe.

Katika miaka mitatu iliyopita tangu kampuni ya Hisense ambayo ni kampuni maarufu ya vyombo vya umeme nyumbani iingie kwenye soko la Misri mwishoni mwa mwaka 2006, chapa ya kampuni hiyo inajulikana zaidi, kiwango cha uuzaji wake wa bidhaa kimeongezeka zaidi, na thamani ya uuzaji iko kwenye nafasi tatu za mwanzo nchini humo. 

Athanas Mang'ati ni Meneja wa Kampuni ya HISENSE Kanda ya Ziwa anasema katika muda mfupi wananchi wameweza kuzielewa bidhaa za kampuni yake na kuzigombania sokoni kutokana na kuja zikiwa za kisasa zenye bei nafuu sanjari na wananchi kuugundua umadhubuti wake yaani ubora, uliokuja na mfumo wa kukidhi mahitaji halisi yanayolingana na hali ya mazingira ya watu wa hali ya juu na wa kipato cha nchini.

Pia mafanikio ya kampuni hiyo yanatokana na wazo la kampuni hiyo la kutengeneza bidhaa zenye chapa yake yenyewe.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.