ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, August 21, 2019

MAONESHO YA 14 YA AFRIKA MASHARIKI YAJA MWANZA.

Mwenyekiti wa TCCIA Dk Elibariki Mmari akizungumza na waandishi wa habari jijini Mwanza.

Wanunuzi zaidi ya laki tatu(300,000) na wafanyabiashara zaidi ya 300 kukutana jijini Mwanza kuanzia tarehe 30Agosti hadi tarehe 8 Septemba, katika maonesho ya bidhaa mbalimbali ya 14 ya Afrika Mashariki.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini humo Mwenekiti wa Chemba ya Biashara,Viwanda na Kilimo (TCCIA) Dk Elibariki Mmari amesema maonesho hayo yana malengo ya kutoa fursa kwa makampuni ya Tanzania na Afrika Mashariki kujitangaza.
‘’Kikubwa ni kutoa fursa kwa makampuni ya Tanzania kujifunza na kukuza wigo wa biashara za nje kati yetu nan chi nyingine kwenye masoko ya Agoa,Eba,Sadc na Jumuiya ya Afrika Mashariki’’ alisema Dk Mmari
Maonesho hayo yatakyofanyika kwenye viwanja vya Rock City mall yana kaulimbiu ya ‘’Kuongeza ubunifu katika uzalishaji na biashara katika kukuza uchumi’’ ambapo bidhaa za nguo,ngozi,ICT,ujenzi, umeme,pembejeo za kilimo bidhaa nyingine ni huduma za kiuhandisi,mbao,bidhaa za kazi za mikono na zawadi.
Ambapo katika maonesho hayo bidhaa zilizopigwa marufuku ni siraha za moto na milipuko,masuala ya kisiasa na mambo ya kidini ambapo hayataruhusiwa kupata nafasi kwenye viwanja hivyo.
Dk Mmari amechukua fursa hiyo kuwakaribisha waoneshaji wa kutoka nje ya Tanzani na kuwakumbusha kulipia vibali vyao kwa wakati kabla ya kusafirisha bidhaa ili kuondokana na usumbufu utakao wakuta.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.