ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, July 17, 2019

ATCL KUANZA SAFARI KUTOKA DAR ES SALAAM HADI MUMBAI, INDIA.


Waziri wa Ujenzi. Mawasiliano na Uchukuzi, Mhandisi Isack Kamwelwe ametangaza kuanzia leo Jumatano, Julai 17 Shirika la ndege la Tanzania (ATCL) litanzindua safari yake ya kwanza kutoka Dar es Salaam hadi Mumbai, India na safari hiyo itaanzia katika Uwanja Mpya wa Ndege wa Kimataifa wa JNIA, Terminal III.

Waziri Kamwelwe alisema hayo mwishoni mwa juma alipokuwa mgeni rasmi katika hafla ya kuadhimisha Siku ya Uhuru wa Taifa la Ufaransa, kwenye makazi ya Balozi wa Ufaransa jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika hafla hiyo Waziri Kamwelwe alisifu uhusiano mzuri uliopo kati ya Tanzania na Ufaransa na kuwakaribisha wawekezaji wa Ufaransa kuja kuwekeza nchini katika sekta za usafirishaji, kilimo, mifugo na uvuvi na kuongeza kuwa Tanzania ni sehemu salama.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.