ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, June 1, 2019

NEMC KUPIGA MZIGO HADI JUMAPILI.



Watendaji  wa Baraza la Taifa la Hifadhi ya Mazingira (Nemc) wametakiwa kutokuwa na mapumziko siku ya kesho badala yake waende sokoni, madukani na magengeni kufuatilia utekelezaji wa katazo la matumizi ya mifuko ya plastiki.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), January Makamba ameyaswema  hayo leo wakati akizungumza na wakazi wa Wilaya Temeke kwenye viwanja vya Zakhem Mbagala kuhusu utekelezaji wa katazo hilo.

Utekelezaji katazo la mifuko ya plastiki limeanza leo baada ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kutangaza Bungeni kutangaza ifikapo Juni mosi mifuko ya plastiki haitakiwi kutumia na kosa kuingiza, kusambaza, kuzalisha na kuiuza.

Kabla ya kuzungumza na wananchi hao, Makamba ambaye pia ni Mbunge wa Bumbuli alifanya ziara ya kutembelea eneo la Kariakoo na kuzungumza na wafanyabiashara mbalimbali kuhusu matumizi ya mifuko mbadala.

"Mtanisamehe sana kesho hakutakuwa na mapumziko  wala sherehe baada jambo hili kuonyesha mafanikio. Msione kazi imeisha mambo ndio kwanza yameenza.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.