ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, March 1, 2019

TCRA YAWA MFANO KATIKA MKUTANO WA TAASISI ZA MAWASILIANO AFRIKA AFRAT



TANZANIA kama ilivyo nchi nyengine duniani, imeshuhudia ukuaji wa sekta ya mawasiliano ambayo imechangia katika kuboresha maisha ya wananchi kijamii na kiuchumi sambamba na pato la taifa.

Ukuaji wa sekta hii umechangiwa na kuwepo kwa sera, sheria kanuni na mfumo mzuri wa utoaji leseni za huduma za mawasiliano.

Sekta hii inachangia katika uchumi moja kwa moja na kwa kupitia sekta ya elimu, afya, kilimo, biashara, ajira, mabenki, utalii, uwekezaji na sekta nyingine zote kama nyenzo ya uwezeshaji katika kuongeza ufanisi wa utendaji kupitia jamii habari.

Tarehe 28 Februari 2019 jiji la Mwanza linakuwa wenyeji wa mkutano wa Baraza la Uongozi la Mawasiliano kutoka Chuo cha Raslimali Watu kwa Maendeleo ya Afrika (AFRALTI) kilichopo Jijini Nairobi nchini Kenya.  ambapo Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella leo anafungua mkutano huo kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano wa Tanzania, Isack Kamwelwe.

Huu ni mkutano unaojumuisha nchi za mbalimbali kutoka Afrika Mashariki na Kusini ikiwemo Tanzania, Kenya, Uganda, Zambia, Malawi, Zimbabwe, Msumbiji, Lesotho na Burundi. wa Mkoa wa Mwanza John Mongella anamwakilisha Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi  kama mgeni rasmi wa mkutano huo.

Fuatilia video kujua yapi yaliyojiri.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.