ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, August 15, 2018

ANGELINE MABULA JIMBO CUP ILEMELA 2018

 Leo jumatatu kata ya buswelu mambo ni moto moto muendelezo wa Mashindano ya ANGELINE MABULA JIMBO CUP 2018 mchuano mkali kati wa watani wa jadi kata buswelu na nyamhongoro katika uwanja wa shule ya msingi buswelu matokeo timu hizo zimetoshana nguvu 2-2 

Kwa niaba ya MH, MBUNGE WA JIMBO LA ILEMELA MGENI RASMI Katibu wa Siasa na Uenezi CHIEF DENNIS LEKELA KANKONO amempongeza Mh, Mbunge wa Jimbo la Ilemela na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Makazi DR. ANGELINE MABULA kwa kuanzisha mashindano hayo kila mwaka na yameleta mafanikio makubwa na kuibua vipaji vya Vijana katika soka na wengine kusajiliwa katika timu za Mbao n.k. 

Pia Katibu huyo amewaomba wadau na Wananchi kumuunga mkono Mh, Mbunge wa Ilemela  katika shughuli mbali mbali za kuleta maendeleo katika Jimbo Ilemela sababu Michezo ni Afya na Ajira!! Mashindano hayo yako katika atua za Makundi ambapo bingwa atanyakua kitita cha sh.milioni _mbili, mshindi wa pili_ sh. milioni moja na nusu na mshindi wa tatu sh. milioni moja. 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.