ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, June 26, 2018

Foundation for Civil Society yakutana Jijini Dodoma na Asasi za Kiraia (AZAKI) inazozifadhili


Meneja Miradi wa Foundation for Civil Society Bw Francis Uhadi akiongea na wana azaki katika mafunzo ya siku tatu ya kuzijengea uwezo asasi za kiraia zinazofadhiliwa na shirika hilo mapema jana jijini Dododma.

Taasisi ya uwezeshaji wa asasi za kiraia ya Foundation for Civil Society (FCS) inaendesha mafunzo ya siku tatu kwa asasi zote inazozifadhili kwa sasa. Mkutano huu wa mafunzo unashirikisha asasi za kiraia (AZAKI) zinazotekeleza miradi ya maendeleo katika maeneo mbalimbali nchini. 

Maeneo haya ni pamoja na uwezeshaji kwa watu wenye ulemavu, vijana, wanawake, haki za raia na demokrasia pamoja na ushiriki wa wananchi katika michakato ya maamuzi, mipango, bajeti, utekelezaji na ufuatiliaji katika sekta za huduma za umma na watendaji wake


Akiongea mapema jana  tarehe 25 juni 2018 kuhusu mkutano huo wa mafunzo, Meneja Miradi wa Foundation for Civil Society Bw Francis Uhadi, amesema mafunzo haya yatachukua siku tatu yakishirikisha asasi 119 kutoka mikoa 22 ya Tanzania Bara na Zanzibar.
“Kuna mambo mengi ya kuongea kwenye agenda, yote yanalenga upitiaji wa mipangokazi na bajeti za miradi yote inayofadhiliwa na Foundation kwa sasa. Na hatua hii huwa tunaifikia baada ya kupitia asasi zote kila mwaka ili kutambua mapungufu ya kiufundi na changamoto nyingine katika utekeleaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ya asasi hizi” ameongeza Bw Uhadi.
Baadhi ya washiriki wakifuatilia kwa umakini semina hiyo.

Imetolewa na Mkurugenzi Mkuu, Foundation for Civil Society 

Kwa kifupi kuhusu Foundation for Civil Society 


FCS ni taasisi iliyo huru isiyo ya kiserikali na wala isiyojiendesha kibiashara iliyojikita kwenye utoaji wa ruzuku na kujenga uwezo kwa asasi za kiraia nchini (AZAKI). Ni kati ya tasisi kubwa za aina hii nchini, Afrika ya Mashariki na Afrika kusini mwa Jangwa la Sahara. Imekua ikifanya kazi ya kujenga AZAKI kwa miaka 15 mpaka sasa.  

Taarifa zaidi,
Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi kupitia: information@thefoundation-tz.org au kupitia namba 0767654252.Unaweza pia kufollow hapa kwa taarifa zaidi - Twitter: @FCSTZ na Facebook: FCSTZ

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.