ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, May 4, 2018

TRA YAANZA RASMI ZOEZI LA KUSAJILI WAMACHINGA MWANZA.


NA ZEPHANIA MANDIA WA G.SENGO TV
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella, ameziagiza halmashauri zote mkoani hapa kuhakikisha asilimia tano za wanawake na vijana, zilizokuwa zikitolewa katika makundi hayo,  zianze kutolewa kwa wafanyabiashara ndogo ndogo (Machinga) ambao wamesajiliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) 

Mongella ametoa agizo hilo wakati wa zoezi la ugawaji wa vitambulisho maalumu kwa wafanyabiashara ndogo ndogo jijini Mwanza waliojiunga katika vikundi mbalimbali vya wajasliamali, ambapo amesema atashangazwa kuona vikundi  ambavyo sio rasmi vikipewa mikopo.

Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato nchini (TRA), Charles Kichere, amewaomba wafanyabiashara wadogo wadogo (Machinga) kujiunga katika vikundi vidogo vidogo ili waweze kunufaika na mikopo mbalimbali inayotolewa na Taasisi za kifedha.

Naibu Kamishna wa kondi za ndani wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Michael Mhoja, amesema mamlaka hiyo tayari imesajili vikundi 30 vya wafanyabiashara ndogo ndogo vyenye jumla ya wafanyabiashara 1,110 huku akidai mpango wao ni kusajili vikundi 130.

Nae Meya wa Jiji la Mwanza, James Bwire akatoa neno kwa wajasliamali hao huku baadhi ya wafanyabiashara hao nao wakazungumzia zoezi hilo.








Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.