ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, May 12, 2018

HARMONIZE AHAMASISHA WAZAZI KUWALEA WATOTO KATIKA MAADILI YA KUTUNZA NA KUTHAMINI MAZINGIRA MWANZA

 Msanii wa muziki wa Bongo Fleva anayetamba na kutikisa Afrika kwa sasa na ngoma yake 'Kwangwaru' Harmonize mapema leo ameshiriki zoezi la upandaji miti katika shule ya Saint Marys iliyoko Igoma Jijini Mwanza.

Akiwa na warembo wa Miss Mwanza takribani 20 alioongozana nao, Harmonize toka WCB amewaasa watoto wadogo wanaosoma katika shule hiyo kuwasikiliza wazazi wao na waalimu akitumia kauli ya wahenga "Asiyesikia la mkuu huvunjika guu" 

"Ninapenda sana watoto kwani ninyi ndiyo furaha ya familia mmenionyesha upendo mkubwa sana kwa kuzifuatilia kazi zangu, Najua mnazipenda kwasababu zinaburudisha na si kupotosha. Natamani sana hapo baadaye nanyi mtimize ndoto zenu" Alisema Harmonize.

Kisha akaongeza "Wazazi wenu wanawapenda ndiyo maana wamewaleta hapa shuleni kupata elimu, nawasihi muwasikilize wazazi wenu pamoja na waalimu wenu kwa umakini na kuwaheshimu kwani asiyesikia la mkuu huvunjika guu, tumeelewanaaaa" Wanafunzi wakajibu kwa pamoja "ndiyooooooo"

Harmonize amewaambia watoto hao kwamba hata yeye asingefika hapo hii leo kwani licha ya kukulia mazingira magumu, kuwaheshimu wazazi wake imekuwa silaha yake kubwa.
 Harmonize amesifia sana hali ya hewa ya jiji la Mwanza akasema inapendezeshwa na watu wake kutunza mazingira.
 Moja kati ya washiriki wa Kinyang'anyiro cha Miss Mwanza ambao wanakwenda kutambulishwa usikuwa 'Hit Zone' akishiriki zoezi la kupanda miti lililoongozwa na msanii Harmonize.
 "Watoto wakilelewa kwenye maadili ya upandaji miti na utunzaji mazingira watakuwa watu wema kwa taifa letu" Asema Harmonize akiwa Shule ya Saint Marry's jijini Mwanza.
 Warembo wote wamepanda miti mahala hapa.
 Rick Junior ni moja kati ya wadau WCB Mwanza naye kapanda mti shuleni hapa.
 Mtoto mtiifu kikazi zaidi.
 Pozi la watoto wetu najua kwa siku za baadaye watajivunia kitu toka eneo hili.
 Mama na wana.....
 Msanii wa muziki wa Bongo Fleva anayetamba na kutikisa Afrika kwa sasa na ngoma yake 'Kwangwaru' Harmonize mapema leo ameshiriki zoezi la upandaji miti katika shule ya Saint Marry's iliyoko Igoma Jijini Mwanza na hapa alikuwa akisaini kitabu cha wageni.
 Mratibu wa Shindano la Miss Mwanza 2018 Pamela akisaini kitabu cha wageni.Mashindano hayo yaliyoandaliwa na Mepal Management Wakala wa Miss Mwanza 2018 , yanatarajia kuzinduliwa hii leo Mei 12 kwenye viwanja hivyo vya Rock City Mall ndani ya show la kibabe la 'Hit Zone Turn Up' lililoandaliwa na kituo cha Redio Jembe Fm Mwanza.
 Picha ndani ya ofisi.
 Maelezo.
 Makaribisho...
 Karibu mgeni.
 Kamati ya Miss Mwanza ikiwaandaa vijana mabalozi wa kesho.
Watoto wakisikiliza kwa makini na utulivu wa hali ya juu.
Historia imeandikwa jijini Mwanza hii leo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.