ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, October 4, 2017

WATAKAOKAIDI BEI ELEKEZI YA MBOLEA KUFIKISHWA KORTINI.

Na Charles Mseti
MAMLAKA ya Udhibiti wa Mbolea nchini (TFRA) imewataka wafanyabiashara wakubwa na wa kati kuzingatia bei elekezi ya uuzaji wa mbolea na uhifadhi wa mbolea kama taratibu za uhifadhi zinavyoelekeza ili wakulima waweze kupata mavuno mengi na kukuza pato la Taifa.

Agousti 18, mwaka huu, Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dk. Charles Tizeba alitangaza bei elekezi ya uuzaji wa mbolea nchini, baada ya kodi mbalimbali za uingizaji wa mbolea kuondolewa ili upatikanaji wake uweze kuwa rahisi zaidi.

Pia imesema mfanyabiashara yeyote yule atakaebainika kuuza mbolea kinyume na bei elekezi iliyotolewa na Serikali kupitia Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, atachukuliwa hatua ikiweni kufikishwa mahakamani mara moja.

Kauli hiyo imetolewa leo na Mkaguzi wa Mbolea wa mamlaka hiyo, Raymond Konga, wakati wa Oparesheni ya kuwabaini wafanyabiashara ambao hawafuati bei elekezi ya uuzaji wa mbolea kwa wakulima, ilioendeshwa jijini hapa.

Konga amesema kuwa wameamua kufanya hivyo ili kukagua kuangalia kama wafanyabiashara wa mbolewa wanafuata bei hiyo elekezi katika kuelekea katika msimu wa kilimo mwishoni mwezi huu.
"Sisi hapa leo tunakagua kama bei elekezi ya mbolea ya kupandia na kukuzia mazoa inafuatwa na kama mlivyojionea wenyewe, baadhi ya wafanyabiashara ikiwemo kampuni ya Matuyuni Agrochemical wao tumebaini wanahifadhi vibaya mbolea yao.

"Baada ya hali hiyo tumeamua kuchukua hatua ya kufunga ghala la kuhifadhia mbolea, kwa sababu mmiliki huyu (Matuyani Laizer) anahifadhi chini ya sakafu kinyume na taratibu zinavyoelekeza uhifadhi wa mbolea lazima iwekwe juu ya mbao," amesema Konga.

Konga amesema ukaguzi huo ambao umeanzia mkoa wa Shinyanga na kuendeshwa katika wilaya zake zote, huku akidai kwamba zoezi hilo ni endelevu kwa mikoa ya kanda ya ziwa na nchini kwa ujumla.

Hata hivyo, amesema lengo la kuendesha oparesheni hiyo kwa wafanyabiashara hao ni kuhakikisha wakulima nchini wanaweza kununua mbolea bora kwa bei elekezi ambayo ni nafuu ili wakulima waweze kupata mavuno mengi.

Mmoja wa wauzaji wa mbolea jijini hapa, Matuyani Laizer, alisema bei hiyo elekezi, itasababisha  nchini kwenda kufa kutokana na wafanyabiashara walio wengi watashindwa kuuza mbolea kwa kuwa hakuna faida wanayoipata kwa uuzaji mbolea huku akiiomba serikali kuangalia upya bei hiyo.

Bei elekezi iliyotolewa na Serikali kwa uuzaji wa mbolea aina ya DAP kwa jiji la Mwanza ni Sh. 55, 438 na mbolea aina ya UREA ni Sh. 42, 859 huku wilaya nyingine za mkoa huo zilizobaki bei ikiwa ni tofauti.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.