ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, September 27, 2017

RC MONGELA ATATUA MGOGORO WA ARDHI ULIOWASHINDA WATANGULIZI WENZAKE TAKRIBANI MIAKA 20 SASA.

NA ZEPHANIA MANDIA WA G.SENGOBLOG TV.


Mkuu wa mkoa wa Mwanza JOHN MONGELA amemaliza mgogoro wa ardhi  uliodumu kwa miaka 20 kwenye mitaa ya Ibanda na Swila kata ya Nyegezi jijini Mwanza hii ikiwa ni kusababisha wananchi wa mitaa hiyo kukosa huduma muhimu za kijamii na kiuchumi ikiwemo shule,soko pamoja na zahanati.



Mgogoro huo ulisababishwa na baadhi ya wananchi kujenga nyumba za makazi kwenye  maeneo ya umma yaliyotengwa kwa ajli ya huduma za kijamii ambapo MONGELA ameamuru huduma hizo zijengwe kwenye  maeneo ambayo hayajaendelezwa. 


Mitaa ya ibanda na swila kata ya nyegezi jijini mwanza haina huduma za kijamii na kiuchumi  baada ya maeneo yaliyokuwa yametengwa  tangu mwaka 1999  kwa ajili ya ujenzi wa shule,zahanati,barabara,soko pamoja na kituo cha polisi kujengwa nyumba za makazi.


Uvamizi wa maeneo hayo umemlazimu mkuu wa mkoa wa mwanza JOHN MONGELA kufika kwenye mtaa wa ibada kwa ajili ya kutafuta ufumbuzi wa suala hilo.



Kufuatia kuendelezwa kwa maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya huduma za kijamii na kiuchumi, MONGELA ameamuru kubadilishwa kwa matumizi ya baadhi ya maeneo ambayo hayajaendelezwa.


Hapa MONGELA akatoa fursa kwa wananchi ambao walifunguka vyema nacho kilio cha malipo ya fidia nacho kikaibuka.

Wananchi wa mitaa ya ibada na swila wamempongeza kwa mkuu wa mkoa wa mwanza JOHN MONGELA kwa kumaliza mgogoro huo uliodumu kwa miaka 18.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.